Kwa mujibu wa shirika la habari la Iran Press, katika mazoezi hayo ya kijeshi vikosi vya wanamapambano wa Hizbullah vimefanya mazoezi ya kushabihisha vita vinavyoweza kutokea baina yao na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.
Ustadi wa kupambana kivita mtu mmoja mmoja, nao pia umeonyeshwa katika mazoezi hayo ya kijeshi ya Hizbullah. Kilichotoa mguso zaidi katika manuva hayo ya harakati ya muqawama ya Hizbullah ni utumiaji wa ndege zisizo na rubani za droni ambazo zitaweza kutumika katika vita vyovyote vile ambavyo vinaweza kutokea katika siku za usoni.
Ndege hizo zisizo na rubani zimepaa katika anga ya kusini mwa Lebanon na kufuatilia harakati na nyendo za wanajeshi wa Israel katika vita mshabaha baina ya utawala huo haramu na Lebanon.
Aidha, bendera za Lebanon na Hizbullah zimepeperushwa angani na ndege zisizo na rubani za Muqawama wa Kiislamu kusini mwa nchi hiyo.
Utumiaji wa ndege zisizo na rubani katika mazoezi ya kijeshi ya Hizbullah kumetuma ujumbe kwamba Muqawama wa Kiislamu wa Lebanon umepiga hatua kubwa za ustawi katika sekta ya kijeshi...
Comments
Post a Comment