Ayatullah Arafi: Dini zote zisimame imara kukabiliana na dhulma za utawala wa Kizayuni wa Israel

 


Mkuu wa vyuo vya kidini nchini Iran amesema: dini zote zinapaswa kusimama imara na kupinga dhulma na ukandamizaji wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.

Shirika la habari la Mehr limeripoti kuwa, Ayatullah Alireza Arafi, Mkuu wa vyuo vya kidini nchini Iran amekutana na kufanya mazungumzo na Mar Awa Royel III Kiongozi mkuu wa Kanisa la Assyrian la Mashariki, ambapo amesisitiza kwa kusema, kutokana na changamoto zinazoikabili jamii ya wanadamu hii leo, dini zinapaswa kutoa mchango chanya na wa ujengaji na akaongeza kuwa: mfumo wa udhibiti na wa dhulma uliopo katika milingano ya kimataifa haukubaliwi na mtu yeyote na kuna ulazima kwa dini zote kuchukua hatua zilizoratibiwa kwa pamoja dhidi ya udhalimu huo.

Ayatullah Arafi amebainisha kuwa: kuporomoka kwa familia ambayo ni kitovu kikuu cha jamii ni mojawapo ya changamoto ambazo dini zinapaswa kuchukua hatua ya kuizuia ili kuepusha ongezeko la madhara na uharibifu wake.
Ayatullah Arafi (kulia) na Mar Awa Royel III

Mkuu wa vyuo vya kidini nchini amesisitiza kuwa: mbali na dini kulinda utambulisho wao, zinapaswa kuelewana na kuchukua hatua za pamoja katika maeneo yanayoziunganisha.

Ayatullah Arafi amesema, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilisimama imara dhidi ya fikra potovu za kundi la kigaidi na ukufurishaji la DAESH (ISIS) na leo hii inasimama imara kukabiliana na utawala wa Kizayuni na akabainisha kwamba: Iran iko bega kwa bega na ndugu zake Waislamu wa Kisuni huko Palestina na inajitoa mhanga katika njia ya kuwatetea wapendwa wake hao, hivyo ni wajibu na jukumu la watu wote kusimama imara na kukabiliana na dhulma za utawala wa Kizayuni wa Israel...

Comments